Mashimba:Hadha ya maji kwisha mkinipa ridhaa October 28

Maswa, Mkoa wa Simiyu

Mgombea Ubunge Jimbo la Maswa Magharibi Ndugu Mashimba Ndaki leo Tarehe 7/10/2020, Saa 8 mchana amefanya mkutano wa hadhara katika kata ya Kadogo kijiji cha Malekano, katika hadhara hiyo.

Amewaahidi wananchi wa kata ya Kadoto kijiji cha Malekano kuwa kama watamchagua na kumchagua Rais John Magufuli kuwa Rais wao. Atahakikisha anatatua kero ya maji na kuwaondolea hadha kwa kufuata maji mbali kwa kuwa kisima kilichopo kina maji yakutosha hivyo akipata ridhaa atahakikisha kuanza na kufunga pump na kujenga kisima kikubwa ili kuwezesha maji kusukumwa na kuweza kuwafikia wananchi wote wa vitongoji vya kijiji cha Malekano.

Katika mkutano huo uliofanyika kata ya Kadogo, kijiji cha Malekano. Mgombea Ubunge Ndugu Mashimba Ndaki amewaomba wananchi kuendelea kuichagua CCM na kumchagua Rais Magufuli kwa kuwa ndie Rais pekee ndani na nje ya CCM anaye tenda anachokiongea.


Comments