Rais
wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Joseph Kabila Kabange,
amewasili hapa nchini jana tarehe 03 Oktoba, 2016 kwa ziara rasmi ya
kiserikali ya siku tatu na kupokelewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Pamoja
na Rais Magufuli viongozi wengine waliompokea Rais Joseph Kabila
Kabange ni Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Wakuu wa
vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi mbalimbali wa Serikali, Mabalozi
na wananchi.
Katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam,
Rais Joseph Kabila Kabange alipokea heshima ya kupigiwa mizinga 21 na
kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake na baadaye
kushuhudia burudani ya vikundi vya ngoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na mgeni wake wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila wakati nyimbo za Taifa za mataifa yote mawili zikipigwa kabla ya ukaguzi wa gwaride lililoandaliwa kwa ajili ya heshima yake.




Comments
Post a Comment