Dr John Pombe Magufuli Ametaganzwa kuwa Ndie Mshindi Kwa Kiti Cha Urais Tanzania

Tume ya uchaguzi ya Tanzania Bara (NEC) kupitia Mwenyekiti wake Jaji Damian Lubuva   imemtangaza  Rasmi  mgombea  Urais  wa  CCM, Dr John Pombe  Magufuli  kuwa  mshindi  halali  wa  kiti  cha  Urais  katika uchaguzi mkuu uliofanyika siku ya jumapili wiki iliyopita.
Kwa  Mujibu  wa  jaji  Lubuva, Dr  magufuli  amepata  ushindi  wa  kura Milioni 8 ( 8,882,935  ) sawa  na  asilimia  58.45%  huku  akimwacha  kwa  mbali  mpinzani  wake  wa  karibu, Edward  Lowassa (Chadema)  ambaye  amepata  jumla  ya  kura  Milioni 6 (  6,077,848  )  sawa  na  asilimia  39.97%

Comments