KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana ameendelea kusisitiza kuwa chama kinarudishwa kwenye misingi yake akitaka mtu anayefikiri misingi hiyo haifai, aondoke atafute mahala pengine.
Kinana ambaye katika ziara zake tangu akiwa Kagera, Geita na sasa
Mwanza, amekuwa akisisitiza viongozi wa CCM kuhudumia wananchi na
kuwatendea haki, alisema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara mjini
Sengerema.
“Nataka niwahakikishe watanzania tunakirudisha hiki chama kwenye
misingi. Na kama kuna mtu anafikiri misingi hiyo haifai, bora aondoke
kwenye CCM atafute mahala pengine pa kwenda,” alisema.
Akishangiliwa na umati wa watu uliohudhuria mkutano huo, Kinana
aliwataka wanasiasa kushikamana kusemea wanyonge. Alisema watu wengi
hawana vyama vya siasa isipokuwa wanalazimika kuingia kutafuta maisha.
Katibu Mkuu alisema wanachotaka ni kuhakikisha chama kinakuwa karibu na watu, kinawasikiliza na kuwasemea.
“Hiki ndicho chama tunachokijua sisi wengine,” alisema na kusihi wana
CCM kushikamana katika kusimamia misingi ya watu kwa kupinga mambo ya
hovyo na kuunga mkono mambo mazuri.
Alisema mtu anayekiri upungufu wake si mtu dhaifu bali ni imara. Alisema si kila jambo linapawa kukubaliwa.
“Watu wananyimwa haki yao, sawa, wanadhulumiwa, tuko mbioni,...nataka
niwahakikishie watanzania, tunakirudisha hiki chama kwenye misingi,”
alisisitiza.
Alisema kazi ya serikali ni kutengeneza mazingira, watu wapate mahitaji yao. Pia alisema serikali inapaswa kusimamia sheria.
Dkt. Nchimbi Atangaza Rasmi Kutogombea Ubunge Songea
Katika hali isiyokuwa ya kawaida baadhi ya wananchi wakiwemo wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma, wamejikuta katika hali ya sintofahamu huku wengine wakimwaga machozi baada ya mbunge wa jimbo hilo, mh. Dkt. Emmanuel Nchimbi kutangaza rasmi kutogombea tena ubunge katika jimbo hilo.
Nchimbi aliyelitumikia jimbo hilo kwa miaka 10 alikutana na wanachama wa chama cha mapinduzi Katika uwanja wa majimaji mjini Songea pamoja
na kuelezea mafanikio mbalimbali ya maendeleo aliyoyafanya katika jimbo
hilo ikiwemo ujenzi wa barabara, zahanati na shule za sekondari lakini
pia akatumia nafasi hiyo kutangaza rasmi kutogombea tena ubunge katika
jimbo la songea mjini.
Tamko
hilo la dkt. Nchimbi lilizua simanzi kwa baadhi ya wananchi na
wanachama wa CCM Songea huku wengine wakishindwa kujizuia na kujikuta
wakimwaga machozi.
Katika
maelezo yao wanachama hawa walisema kuachia ngazi kwa Dkt, Nchimbi
kutogombea katika jimbo hilo kunatoa fursa kubwa kwa vyama vya upinzani
kuchukua jimbo hilo hali ambayo hawakubaliani nayo.
Hata
hivyo wanachama hao walimuomba mbunge huyo kutengua msimamo wake na
kumtaka arejee tena kugombea jimbo la Songea mjini, jibu la dkt. Nchimbi
likawa anaenda kufikiria.


Comments
Post a Comment